- Kushiriki kikamilifu katika shughuli za Chama ikiwa ni pamoja na kuhudhuria mikutano yote inayohusika;
- Kushiriki katika kutoa uamuzi wa mambo mbalimbali katika Mikutano Mikuu;
- Kupiga kura chini ya misingi ya mtu mmoja kura moja bila kujali idadi ya Hisa anazomiliki;
- Kuchagua na/au kuchaguliwa katika Uongozi wa chama.
- Kuwa na haki sawa kuhusu mali ya Chama na kudhibiti ipasavyo matumizi yake;
- Kupatiwa huduma zozote zinazotolewa na chama ilimradi amekidhi masharti yanayoambatana na huduma hiyo;
- Kupatiwa taarifa mbalimbali za utekelezaji wa shughuli za Bandarini SACCOS, muhtasari wa mkutano na nyaraka nyingine za chama kwa ajili ya mapitio akiwa katika ofisi za chama;
- Kuteua Mrithi;
- Kupokea gawio na faida nyingine kutoka katika shughuli za chama kwa kuzingatia masharti.